Serikali imeitaka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) kuharakisha mchakato wa kupata ithibati ya kimataifa (International Accreditation) kwa ajili ya maabara yake ya Chakula na Lishe iliyopo Mikocheni, jijini Dar es Salaam.
Hatua hiyo inatajwa kuwa itafanya Tanzania kuwa kitovu cha utoaji wa huduma za chakula na lishe zinazokidhi viwango vya kidunia, huku ikifungua milango mipana ya masoko na ushirikiano wa kimataifa.
Wataalamu wa Lishe kutoka Wizara ya Afya Zanzibar na Wizara ya Elimu Zanzibar, Mei 5, 2026, wametembelea Maabara ya Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) iliyopo Mikocheni jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kujifunza uzoefu wa uchambuzi wa sampuli mbalimbali zinazohusiana na vyakula.
Maabara ya TFNC ni Maabara Rejea inayotambulika na kuaminika kimataifa na mashirika kama WHO, CDC, ECSA-HS, na IGAD, ikiwa ni maabara pekee ya aina yake katika ukanda wa Afrika Mashariki, Kati, na Kusini.
Tarehe 28 Aprili ,2025, Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) kwa kushirikiana na Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) wameanza kutoa mafunzo maalum ya matumizi ya mbinu mpya ya MIMI (Modeling and Mapping Risk of Inadequate Micronutrient Intake) ikiwa ni mwendelezo wa jitihada za kujenga uwezo wa kitaifa kwa wataalamu katika suala la uchambuzi wa takwimu zinazohusu athari za Viashiria vya upingufu wa Vitamini na Madini
Serikali imeitaka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) kuharakisha mchakato wa kupata ithibati ya kimataifa (International Accreditation) kwa ajili ya maabara yake ya Chakula na Lishe iliyopo Mikocheni, jijini Dar es Salaam. Hatua hiyo inatajwa kuwa itafanya Tanzania kuwa kitovu cha utoaji wa huduma za chakula na lishe zinazokidhi viwango vya kidunia, huku ikifungua milango mipana ya masoko na ushirikiano wa kimataifa.