Kamati ya Taifa ya Wataalam ya Usimamizi na Ushauri wa Masuala ya Lishe imekutana tarehe 16 Machi 2026 katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Jijini Dodoma, kujadili na kufanya tathmini ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali za lishe nchini ikiwemo Mpango Jumuishi wa kitaifa wa masuala ya lishe pamoja na mikakati mingine ya kuboresha hali ya lishe nchini.
Wakizungumza wakati wa kikao kazi cha kuthibitisha mpango huo kilichofanyika Mkoani Morogoro, wadau mbalimbali walioshiriki kwenye kikao hicho wameipongeza Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Pamoja na timu iliyoshiriki katika kuandaa mpango huo hadi kufikia hatua ya mwisho kwani unaenda kusaidia kuimarisha eneo la urutubishaji nchini, na ni mpango ambao wadau wengi wa urutubishaji walikuwa wanauhitaji.
Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania kwa kushirikiana na Wadau wengine wa urutubishaji kupitia ufadhili wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) wako mbioni kukamilisha program ya kitaifa ya urutubishaji wa vyakula ikiwemo uwekaji wa madini joto kwenye chumvi.
Kamati ya Taifa ya Wataalam ya Usimamizi na Ushauri wa Masuala ya Lishe imekutana tarehe 16 Machi 2026 katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Jijini Dodoma, kujadili na kufanya tathmini ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali za lishe nchini ikiwemo Mpango Jumuishi wa kitaifa wa masuala ya lishe pamoja na mikakati mingine ya kuboresha hali ya lishe nchini.