Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya tathimini ya lishe, unasihi na huduma za lishe kwa Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI na TB wakifanya jaribio la awali kwa ajili ya kupima uelewa wao kabla ya kuanza mafunzo hayo. Mafunzo haya yanatolewa kwa siku nne (25 - 28, Novemba, 2025) na TFNC kwa watoa huduma za afya, maafisa usawi na maaendelo ya jamii ili kuwaongezea ufanisi katika majukumu yao ya kila siku.
Wafanyakazi wa Maabara ya Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), wamepatiwa mafunzo ya kanuni bora za ufanyaji Kazi kwenye maabara yaani GLP na GCLP, ikiwa ni sehemu ya kuboresha usimamizi, ubora na usalama katika Maabara ya Chakula na Lishe iliyopo Mikocheni jijini Dar es Salaam. Mafunzo hayo yametolewa na mwezeshaji Prof. Reginad Kavishe kutoka KCMC University na yamefanyika mkoani Morogoro katika Chuo cha Kilimo cha Sokoine.
Oktoba 6,2025 Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) imepokea wageni kutoka Chuo Kikuu cha Eduardo Mondlane, Wizara ya Uchumi na Wizara ya Afya kutoka nchini Msumbiji, kwa lengo la kujifunza na kupata maarifa juu ya utekelezaji wa mpango wa kuzuia upungufu wa madini joto ( USI) kama mkakati wa muda mrefu wa kuzuia na kudhibiti upungufu wa madini joto mwilini.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya tathimini ya lishe, unasihi na huduma za lishe kwa Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI na TB wakifanya jaribio la awali kwa ajili ya kupima uelewa wao kabla ya kuanza mafunzo hayo. Mafunzo haya yanatolewa kwa siku nne (25 - 28, Novemba, 2025) na TFNC kwa watoa huduma za afya, maafisa usawi na maaendelo ya jamii ili kuwaongezea ufanisi katika majukumu yao ya kila siku.