Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, ametembelea Banda la Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), wakati wa Mkutano Mkuu wa Wadau wa Lishe uliofanyika katika kituo cha Mikutano cha APC Bunju jijini Dar es Salaam.
akiwa katika banda hilo, Mhe. Majaliwa amepata maelezo kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania kutoka kwa Mkurengezi Mtendaji wa TFNC Dkt. Germana Leyna.