Timu ya Watafiti bobezi kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), Iodine Global Network (IGN), pamoja na Shirika la Nutrition International (NI) wametoa mafunzo elekezi kwa Waganga wakuu, Maafisa Lishe, Waratibu wa Mama na Mtoto, Wauguzi, Wataalamu wa Maabara na Wataalamu wa taarifa za afya na lishe wa Halmasauri ya Meatu mkoani Simiyu, ikiwa kuwaandaa tayari kushiriki kwenye utafiti wa FORTIMAS.