Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Kinga Wizara ya Afya, Dkt. Otilia Gowele akiwasilisha salamu za Wizara ya Afya katika Mkutano wa 39 wa Jukwaa la Wadau wa Uongezaji Virutubishi kwenye Vyakula nchini Tanzania (TFFA), unaofanyika kwa muda siku mbili jijini Arusha ukiwakutanisha wadau mbalimbali wanaojihusisha na masuala ya urutubishaji wa vyakula wakiwemo kutoka Wizarani, Taasisi za Serikali, Vyuo Vikuu, Mashirika ya Maendeleo pamoja na wadau wengine.