Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Grace Magembe amemtaka Mkurugenzi wa Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto Dkt. Ahmad Makuwani pamoja na viongozi wengine wa Wizara ya Afya kwa kushirikiana na OR-TAMISEMI, kusimamia Mpango wa kuanzishwa matumizi ya virutubishi lishe kwa uadilifu, umahiri na kwa kuzingatia mahitaji ya wajawazito hapa nchini.