Mafunzo ya Uandaaji Bora wa Chakula kwa Watoa Huduma ya Chakula
07 Feb, 2026

Bonyeza hapa ili kujisajili: Bonyeza Hapa Kujisajili

 

Mafunzo ya Uandaaji Bora wa Chakula kwa Watoa Huduma ya Chakula

Malengo ya Mafunzo

  • Kuongeza kipato kwa kuboresha stadi za kutayarisha chakula zinazohifadhi virutubisho.

  • Kuongeza uelewa kwa vitendo kuhusu mbinu bora za maandalizi ya chakula katika kukabiliana na uzito ulio kithiri, unene, magonjwa yasiyoambukiza na magonjwa ya mlipuko.

  • Kujenga uwezo katika kanuni za usafi wa chakula, matumizi sahihi ya vitendea kazi, hifadhi sahihi ya chakula, na kupunguza hasara na athari zinazotokana na uchafu wa chakula.

MUHIMU:
Mafunzo haya yatawasilishwa kwa nadharia na vitendo.


Mahali: Morogoro
Tarehe: 11–12 Februari, 2026
Mwisho wa Kujisajili: 09 Februari, 2026

Ada: Tsh 200,000
(Ada hii inajumuisha gharama za chakula na cheti)

Kujisajili tembelea: https://www.tfnc.go.tz

Kwa mawasiliano zaidi piga:
+255 623 752 053 / +255 683 467 454