Watafiti wa TFNC wajengewa uwezo
Imewekwa: 30th Nov, 2024
Watafiti wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) Novemba 28, 2024, wamejengewa uwezo wa namna ya kuandika maandiko yenye ushawishi na ushindani wa kupata fedha za kufanya tafiti mbalimbali zinazohusiana na masuala ya Chakula na Lishe.
Semina hiyo imewezeshwa na Prof. Elia Mmbaga kutoka Chuo Kikuu cha Oslo Norway.