Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Bi. Sofia Kizigo amemwakilisha Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu katika ziara ya kuangalia shughuli zinazofanyika katika Siku ya Afya na Lishe ya Kijiji wilayani humo, ziara ambayo imeratibiwa na Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania kupitia ufadhili wa WFP.
Wito umetolewa kwa kina baba kuhudhuria kwenye maadhimisho ya Siku ya Afya na Lishe ya Kijiji (SALIKI) ili waweze kushiriki kupatiwa elimu ya lishe pamoja na huduma mbalimbali zinazohusiana na afya na lishe ili waweze kushiriki katika kusimamia lishe za watoto wao na kutengeneza kizazi chenye lishe bora.
Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma Bi. Sofia Kizigo wakati aliposhiriki kwenye utekelezaji wa Siku ya Afya na Lishe ya Kijiji (SALIKI), akimwakilisha Waziri wa Afya Mhe.Ummy Mwalimu, na kujionea shughuli mbalimbali zinazofanyika katika siku hiyo ambayo utekelezwa kila baada ya miezi mitatu.
|