09 Sep, 2025
Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania kwa kushirikiana na Mpango wa Chakula Duniani (WFP) imetoa mafunzo ya usindikaji wa chakula cha nyongeza kwa kutumia mazao yaliyoongezwa virutubishi kibailojia. Mafunzo hayo ambayo yametolewa na wataalamu kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzani, yamehusisha vikundi mbalimbali vya wanawake mkoani Singida.
