Kikao cha utambulisho wa Msimamizi Mkuu mpya wa shughuli za lishe nchini kutoka UNICEF

Imewekwa: 3rd Mar, 2022
Na, Jackson Monela - Ofisi ya Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania,Dar es salaam , Tarehe 02.03.2022.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Dkt. Germana Leyna (mwenye koti jekundu) pamoja Msimamizi Mkuu mpya wa Shughuli za lishe nchini kutoka Shirika la Kuhudumia Watoto la Umoja wa Mataifa (UNICEF) Patrick Codjie (wa sita kutoka kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania mara baada ya kumalizika kwa kikao cha utambulisho wa Bw.Patrick Codjie juu ya shughuli zinazofanywa na Taasisi pamoja na zile zinazofadhiliwa na Shirika hilo katika mwaka wa fedha 2021-22 pamoja na maeneo yatakayofadhiliwa kwa mwaka ujao wa fedha wa 2022-23.