Mafunzo ya Usindikaji Unga Mchanganyiko kwa matumizi ya Watoto wenye umri wa miezi 6-23
21 Apr, 2026

USAJILI :  BONYEZA HAPA KUJISAJILI

 

Mada zitakazofundishwa:

  • Masuala ya msingi kuhusu chakula cha nyongeza kwa watoto
  • Uongezaji wa virutubishi kwenye vyakula Tanzania
  • Kanuni bora za usindikaji wakati wa kuandaa unga mchanganyiko:
    • Mbinu za kupunguza sumu kuvu
    • Mbinu za kuzuia vimelea vya magonjwa
  • Hatua za usindikaji wa unga mchanganyiko kwa kutumia mazao ya kawaida na yaliyoongezwa virutubishi kibailogia 
  • Aina za michanganyiko ya unga

Walengwa wa mafunzo: Wajasiliamali wanaosindika vyakula vya watoto wenye umri wa miezi 6 hadi 23. 

Sifa za mwombaji: Awe na uwezo wa kusoma na kuandika

Lugha ya mafunzo: Kiswahili

Tarehe: 22–24 Mei 2026

Mahali: TFNC – Mikocheni (Mtaa wa Sembeti)

Ada: TZS 160,000
(Inajumuisha chakula, ukumbi na cheti)